Wednesday, October 24, 2012

KHAMIS SADIFA JUMA AULA UENYEKITI WA UVCCM TAIFA.


Dk. Sheni akimpongeza Khamis Sadifa Juma, baada ya kutangazwa Mshindi wa kuwa Mwenyekiti mpya wa UVCCM Taifa, katika uchaguzi uliofanyika jana mjini Dodoma. (Picha na Bashir Nkoromo).
Mjumbe wa Kamati Kuu, Rais wa Zanzibar, Dk. Shein akiwa na Mwenyekiti mpya wa UVCCM,  Khamis Sadifa Juma na Makamu Mkt UVCCM, Mboni Mhita baada ya viongozi hao wapya wa Umoja huo kutangazwa kuwa washindi leo katika uchaguzi mkuu wa UVCCM uliofanyika jana mjini Dodoma. 
 Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti UVCCM Beno Malisa akimpongeza Khamis Sadifa Juma, baada ya kutangazwa Mshindi wa kuwa Mwenyekiti mpya wa UVCCM Taifa, katika uchaguzi uliofanyika jana mjini Dodoma.
Kamanda wa Chipukizi Kingunge Ngombale-Mwiru akijadili jambo na Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama wakati wa kutangazwa matokeo.
Katibu Mkuu wa UVCCM Martine shigela akimkaribisha meza kuu Khamis Sadifa Juma bada ya kutangazwa mshindi.
Khamis Sadifa Juma

No comments:

Post a Comment

KIJIWENI BONGO HAITAUSIKA NA MAONI YANAYOWEKWA NA WASOMAJI